Tuesday, February 05, 2019
Sunday, February 03, 2019

Simba SC Yaburuzwa Bao 5-0 Dhidi ya Al Ahly

Katika michezo wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika, katika kundi D jana ndani mji wa Alexandria Misri kulipigwa mtanange mkali uliozikutanisha timu ya Simba SC ambao walikuwa ugenini kuchuana na Al Ahly.
katika dakika 90 za mchezo huo Simba iliweza kuruhusu alama tatu kwenda kwa timu ya Al Ahly baada ya kukubali kichapo cha bao 5- 0, ambapo magoli yote yalifungwa ndani ya kipindi cha kwanza.
kikosi cha simba kimekuwa na mwendelezo wa kufungwa bao tano kwa sifuru baada ya kupigwa na AS Vita nchini Congo, Simba inaendelea kushika nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi kundi D ikiwa na jumla ya alama 3 huku Al Ahly ikizidi kujiimarisha kileleni ikiwa na jumla ya alama 7 huku As Vita ikishika nafasi ya pili baada ya jana kutoa sare ya mabao 2- 2 na JS Saoura, na kuifanya JS Saoura iendelea kuburuza mkia katika kundi hilo .
Saturday, February 02, 2019
Friday, February 01, 2019
Mechi Zitakazochenzwa Leo Ligi Kuu Bara, TPL
Kagera Sugar watacheza na kikosi cha Tanzania Prisons Uwanja wa Kaitaba, KMC wapo mkoani Shinyanga watacheza na Stand United uwanja wa Kambarage.
JKT Tanzania wataikaribisha Mwadui uwanja wa Isamuhyo na Ruvu Shooting leo atakuwa kazini kumenyana na Mbeya City uwanja wa Mabatini.























































